Na Woinde Shizza ,Arusha 

Chama cha  wanunuzi na wauzaji wa Madini Tanzania TAMIDA kimetoa tamko la kulaani  kitendo cha uongozi wa  Haliamshauri ya Simanjiro  kuwavamia wafanyabiashara wa madini  wa jijini Arusha maofisini wakiwa wameambatana na Askari wenye silaha za moto na pingu  kuwalazimisha kulipa  kodi ya tozo ya huduma ya Madini.

Akitoa tamko hilo katika mkutano wa wafanya biashara wa Madini uliofanyika katika Ofisi za wizara ya madini Kanda ya Kaskazini jijini hapa  Makamu  mwenyekiti wa TAMIDA Thomas Munis alisema kitendo hicho hakikubaliki na kimelenga kuwadhalilisha wafanyabiashara hao pamoja na wateja wao.
Thomas aliutaka uongozi wa Wilaya ya Simanjiro kukaa chini na kukubaliana  namna ya ulipaji wa tozo hiyo inayofikia kiasi cha shilingi Milioni 20 hadi 60 kwa mwaka, jambo ambalo alisema hawawezi kulipa mara mbili kwa halimashauri ya Arusha pamoja na Halimashauri ya Simanjioro.
"Sisi kama wafanyabiashara hatupingi kulipa kodi yoyote ya madini ila tunachosikitishwa nacho ni hatua ya uongozi wa Simanjiro kutufuata maofisini wakiwa na silaha za moto na pingu, kutaka tulipe kodi huduma ambayo kimsingi tumekuwa tukilipa kila mwaka katika halimashauri ya Arusha", Alisema Thomas.
Aidha aliongozea kusema kuwa wao kama wafanyabiashara wa madini hawapingi kulipa kodi yoyote inayotozwa kutokana na biashara ya madini ila wanachopinga kodi hiyo kutozwa mara mbili kwa mwaka katika halimashauri zote swala ambalo wameliomba serekli kupitia wizara ya madini kuingilia kati swala hilo na kutatua mkanganyiko huo.

Wakati huo huo afisa madini kutoka ofisi hiyo ya kanda Bwana Erick Mpesa amesema kuwa wao kama  kama wasimamizi wa madini katika kanda hii wanangoja maafikiano ya pande zote mbili ikiwemo halmashauri ya Simanjiro pamoja na jiji la Arusha juu ya Tozo hiyo ya huduma ya Madini.
Kwa upande  mwanasheria Jiji la Arusha  Bahati Chojo amesema kuwa sheria inaelekeza wazi kuwa  kampuni yoyote inayofanya biashara ya madini inapaswa kulipa tozo ya huduma kule ilipo ikiwemo kulipa kule ilipo ofisi pamoja na maeneo ya matawi ya ofisi hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...