
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Kwa
miaka mingi hapa nchini Tanzania, Kilimo kimetajwa kuwa uti wa mgongo
wa Taifa. Ikumbukwe kuwa miaka ya Sabini za mwanzoni kuliwahi kuwepo
kauli kuhusu kilimo iliyosema “Kilimo cha Kufa na Kupona”. Kauli hii
ililenga kuondoa njaa iliyokuwa inalikabili Taifa. Kwa miaka ya
hivi karibuni, serikali ikaja na Kauli Mbiu ya “Kilimo Kwanza”. Hizi
zote ni jitihada za kuinua kilimo ambacho kinategemewa na walio wengi
hapa kwetu.
Kilimo ni eneo la kipaumbele katika uchumi wa Tanzania licha ya kuwa kilimo nchini bado kinategemea kwa kiasi kikubwa mvua na hali ya hewa kwa ujumla .
Kwa mujibu wa taarifa za mamlaka ya hali ya hewa iliyotolewa na Mkurugenzi
Mkuu Dkt. Agnes Kijazi zinasema mvua za masika zimeshaanza katika
maeneo mengi yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka. Mvua hizi
zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani katika maeneo mengi.
Hata hivyo maeneo machache yanatarajiwa kupata mvua za wastani hadi
chini ya wastani.
Hali
ya unyevunyevu wa udongo inatarajiwa kuwa ya kutosheleza shughuli za
kilimo katika maeneo mengi.Hata hivyo, mvua za juu ya wastani
zinazoendelea kunyesha zinaweza kusababisha hali ya unyevunyevu wa
udongo kupita kiasi hivyo kuathiri mazao na hata kusababisha mafuriko na
kuharibu mazao.
Kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, msimu wa mvua za Masika katika
kipindi cha miezi ya Machi hadi Mei, 2016 ni mahususi katika maeneo ya
Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki (Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na
Manyara), Pwani ya Kaskazini, (Mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani,
Morogoro-Kaskazini pamoja na Visiwa vya Unguja na Pemba), Kanda ya Ziwa
Victoria (Mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza, Geita, Simiyu na Shinyanga) na
kaskazini mwa mkoa wa Kigoma. Mvua hizo zinatarajiwa kuwa za wastani
hadi juu ya wastani kwa maeneo mengi ya ukanda huo isipokuwa maeneo ya
Kusini mwa ukanda huo yanatarajiwa kuwa na mvua za wastani hadi chini ya
wastani.
Kutokana
na mvua zinazoendelea kunyesha tahadhari imetolewa kwa wakulima wote
kuwa makini na mvua hizi za masika zinazoendelea kwani zinatarajiwa
kunyesha kwa wingi katika baadhi ya maeneo kulingana na uelekeo wa upepo
katika maeneo mengi ambayo yanayopata mvua za msimu wa masika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...