Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akiongoza kikao kilichoshirikisha Watendaji kutoka Benki ya Dunia pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini na taasisi zake ikiwa ni pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) na Wakala wa Serikali wa Uagizaji wa Mafuta ya Pamoja (PBPA).
Mtendaji Kutoka Benki ya Dunia anayeshughulikia mazingira Vladislav Vucetic, akielezea mikakati ya benki hiyo katika ushirikiano wake na Serikali ili kupanua sekta za nishati na madini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa (kushoto waliokaa mbele) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati Dkt. Juliana Pallangyo ( wa pili kutoka kushoto waliokaa mbele) wakifuatilia kwa makini maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo( hayupo pichani) katika kikao hicho.
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ameelezea mikakati ya Serikali katika uboreshaji wa sekta za nishati na madini na kuongeza kuwa Serikali ipo tayari kushirikiana na Benki ya Dunia (WB) katika uboreshaji wa sekta hizo ili ziwe na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi.
Profesa Muhongo aliyasema hayo alipokutana na Watendaji kutoka Benki ya Dunia pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini na taasisi zake ikiwa ni pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) na Wakala wa Serikali wa Uagizaji wa Mafuta ya Pamoja (PBPA).
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...