Mwenyekiti wa McAlister Consulting Corporation na Balozi mstaafu wa Canada nchini Tanzania Balozi Andrew McAlister akizungumzia uzoefu wake kuhusiana na uwekezaji na uwajibikaji wa kampuni za madini, gesi na mafuta katika mkutano wa kikanda iliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi leo jijini Dar es Salaam yenye malengo ya kupunguza migogoro kati ya kampuni hizo na jamii zilizopo katika maeneo yao ya uwekezaji.
Makamu wa Rais Mwandamizi wa kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia Mining Plc Bw. Deodatus Mwanyika (kulia) akichangia mjadala katika mkutano wa kimataifa wa kikanda kuhusu Leseni za Kijamii za Uendeshaji iliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi mapema leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili namna ambavyo wawekezaji katika sekta ya madini, gesi na mafuta wanaweza wakaongeza uwajibikaji na kupunguza migogoro kati yao na jamii zinazowazunguka katika maeneo yao ya biashara. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa TCME Balozi Ami Mpungwe, Mwezeshaji wa mkutano huo Bw. Aidan Eyakuze na Mbunge na Mwenyekiti wa Fedha ya Bunge kutoka nchini Ghana Mhe. James Avedzi.
Mtaalam wa kimataifa wa Leseni za Kijamii za Uendeshaji Dkt. Ian Thomson, akiwasilisha mada kuu katika mkutano wa kikanda iliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi leo jijini Dar es Salaam kuhusiana na namna ambavyo wawekezaji wa madini, gesi na mafuta wanaweza wakajitahidi kuongeza kiwango chao cha kukubalika na kupunguza migogoro kati yao na jamii zilizopo katika maeneo yao ya uwekezaji.
aafisa waandamizi wa serikali, sekta binafsi, taasisi zisizo za kiserikali na taasisi za elimu wakishiriki mkutano wa kikanda kuhusu Leseni za Kijamii za Uendeshaji iliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili namna ambavyo wawekezaji katika sekta ya madini, gesi na mafuta wanaweza wakaongeza uwajibikaji na kupunguza migogoro kati yao na jamii zinazowazunguka katika maeneo yao ya biashara.







Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...