WITO WA KUTOA MAONI KUHUSU MUSWADA 
WA SHERIA YA MANUNUZI.
Katika kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia matakwa ya Kanuni ya 117 (9) ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Januari 2016; Kamati ya Bunge ya Bajeti imepanga kufanya mkutano wa kusikiliza maoni ya wadau wote wa masuala ya Ugavi (Public Hearing) kuhusu Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma wa Mwaka 2016(Public Procurement Act 2016) kabla Muswada huo haujapitishwa na Bunge kuwa Sheria .
Mkutano huo wa kusikiliza maoni ya wadau (Public Hearing) unatarajiwa kufanyika  siku ya Jumatatu Juni 27, 2016 Bungeni Dodoma kuanzia saa Tano Asubuhi katika Ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni - Dodoma.

Kwa kuzingatia umuhimu wa Muswada huo, Kamati inawaalika wadau wote kufika na kuwasilisha maoni yao mbele ya Kamati kabla kupelekwa katika hatua nyingine. Maoni ya wadau yanaweza pia kuwasilishwa kwa njia ya Posta au Barua pepe kwa anuani ifuatayo:

Katibu wa Bunge,
Ofisi ya Bunge,
S.L.P. 941,
DODOMA
Barua pepe: cna@bunge.go.tz

Imetolewa na,
Kitengo cha Habari, ElimunaMawasiliano.
Ofisi ya Bunge,
S.L.P 941, 
DODOMA
24 Juni, 2016.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...