Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na walemavu, Mh. Jenista Mhagama akizungumza na maafisa wa GEPF wakati alipotembelea banda lao katika viwanja vya Maonyesho ya biashara ya kimataifa ya 40 (Sabasaba) Jijini Dar es salaam, na kupatiwa maelezo ya jinsi Mfuko ulivyofanikiwa kutoa huduma kwa wajasiriamali.
Mh Jenista Mhagama akitia saini kitabu cha kumbukumbu za wageni waliopita katika banda la GEPF.
Uzinduzi wa Boda boda Scheme ulivutia wadau wengi wa sekta ya hifadhi ya jamii nchini. Pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof. Godius Kahyarara baada ya kupata maelezo ya mafanikio ya Boda Boda Scheme kutoka kwa Afisa masoko Bw Valence Masebu.
wajasiriamali (Mama lishe) wakijaza fomu za kujiunga na mpango maalum wa kujiwekea akiba ya uzeeni (VSRS) huku wakipatiwa maelezo na Afisa Masoko Bw Avit Nyambele.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...