Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe mkoani Kihoma, Kanali Marco Gaguti akizungumza leo wakati wa mafunzo ya siku moja kwa watendaji wa halamshauri mbili za Buhigwe na Uvinza ambazo zimechaguliwa kuanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya sekta za Umma (PS3) unaofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika lake la Misaada la Kimataifa (USAID).
Kanali Gaguti aliwataka watumishi hao wa halmashauri hizo mbili kuchukulia fursa hiyo ya kuanza utekelezaji wa ,radi huo kwa umuhimu kubwa kwani kuanza kwao ni kutokana na changamoto zilizipo katika Halmashauri zao.
"Tutumie fursa hii kikamilifu ili kukabiliana na changamoto zilizopo katika halmashauri zetu, tumeona kuwa tuna miradi mingi katika maeneo yetu lakini hatuitumii vizuri kutusaidia hivyo tuanze mradi huu wa PS3 kwa kumbukumbu kwa kupiga hatua nzuri ili tuondoke hapa tulipo katika changamoto,"alisema Kanali Gaguti.
Mshauri wa Masuala ya Fedha wa PS3, Victor Msoma akizungumza jambo baada ya mawasilisho ya Halmashauri.
Mwakilishi wa Halamashauri ya Buhigwe, ambaye ni Afisa Elimu ya Msingi, Mwl. Freddy Fande akiwasilisha taarifa ya Halmashauri hiyo.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, Benard Rusomyo akiwasilisha taarifa ya Wilaya yake.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...