Na Mathias Canal, Singida
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu ametangaza rasmi siku ya Jumatano kuwa siku ya kazi za pamoja katika majengo ya Umma katika Vijiji vilivyopo Wilayani humo.
Tangazo hilo amelitoa kwenye halfa iliyofanyika katika ukumbi wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida wakati anakabidhiwa ofisi na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo ambaye kwa sasa amestaafu Gishuli Charles.
Mtaturu amesema kuwa Uongozi utachagua kama ni Shule, Zahanati au Utengenezaji wa Barabara n.k.ambapo Wananchi wote watapaswa kushiriki kazi hiyo ili warejeshe moyo wa kushiriki shughuli za maendeleo ambapo mkuu huyo amesema yeye atafanya kazi ya kupita katika maeneo tofauti kuungana na Wananchi katika kukamilisha kwa vitendo jambo hilo..
Amewakumbusha wananchi kuwa wakati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na wenzake waliokuwa wanaanza harakati za kudai Uhuru walienda Umoja wa Taifa wakahakikisha tunaweza kujitawala na kujisimamia wenyewe bila mkoloni.
Mwaka 1961 tulipopata Uhuru Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alieleza sasa tumepata uhuru tubadili malengo ya Taifa iwe ni Uhuru na Kazi aliamini kupitia kazi tutapata maendeleo.
Awamu ya Tano imekuja na kauli mbiu ya “HAPA KAZI TU”; kwa maana hiyo hiyo kuhimiza Wananchi kufanya kazi na kazi ndio kipimo cha utu.
Mkuu huyo amesema kuwa wananchi wote wanapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kuboresha maisha ya kila mmoja na familia zetu kwa ujumla.
Mkuu huyo amesema kuwa Kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi mwaka 2015 – 2020. Ibara ya 49 imeeleza Serikali kuongeza huduma za Afya, kuongeza Wataalamu wa Afya kwenye Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali za Wilaya n.k.
Amesema Ilani imetambua yaliyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Nne katika Sekta ya Afya kama msingi wa kuendeleza juhudi zaidi kupiga vita Malaria, UKIMWI, Vifo vya Mama na Mtoto n.k. Uboreshaji na upatikanaji wa dawa na vifaa tiba.
Katika Wilaya ya Ikungi kuna upungufu wa asilimia 62% ya Zahanati hivyo kufanya akina Mama Wajawazito kutembea mwendo mrefu kufuata ushauri wa kitaalamu.
Huduma ya kuzuia maambukizi ya VVU kwenda kwa mtoto (PMTCT) vimeongezeka ila bado havitoshi; Vituo vya tiba vya maangalizi ya wanaoishi na VVU (CTC) bado ni vichache sana.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida Mhe. Miraji Jumanne Mtaturu wakikabidhiana nyaraka na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo ambaye kwa sasa amestaafu Mhe. Gishuli Charles.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe. Miraji Jumanne Mtaturu akiwa ofisini kwake mara baada ya kukabidhiwa ofisi na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo ambaye kwa sasa amestaafu Mhe. Gishuli Charles.
Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo ambaye kwa sasa amestaafu Mhe. Gishuli Charles na baadhi ya viongozi wa wilaya hiyo wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe. Miraji Jumanne Mtaturu





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...