Mkuu wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Mhe. Asia Juma Abdallah leo ametembelea zahanati ya Kilolo mapema asubuhi kwa lengo la kujionea mazingira ya zahanati hiyo.
Akiwa hapo alikutana na Daktari mfawidhi Dkt. Selemani Jumbe ambapo pamoja na mambo mengine alimwambia kuwa wanatamani sana kuwa na vifaa vya kufanyia kazi kama vile Full Blood Picture Machine, Ultra Sound, Na X-ray ambavyo anasema kwa wilaya nzima hakuna huduma ya X-ray hivyo inawawia vigumu kukamilisha tiba kwa wagonjwa wenye kuhitaji huduma hiyo.
DC Asia pia alikutana na wazee wa mji wa Kilolo ambao wameiomba serikali kuwapatia watalaamu pamoja na vifaa vya upasuaji kwa kuwa tayari walishapata jengo la upasuaji kutoka kwa mdau wa maendeleo ila wanakwama kuanza kutumia huduma hiyo ya upasuaje kufuatia ukosefu huo wa wataalamu na Vifaa.
Mhe Mkuu wa Wilaya huyo aliwaahidi kufuatilia na kutafuta ufumbuzi wa changamoto hizo, huku akitoa wito kwa wananchi kuendelea kutunza miundombinu iliyopo wilayani humo kwa faida yao
Mkuu wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Mhe. Asia Juma Abdallah akiwa na Dkt. Selemani Jumbe mwenye koti jeusi na Bw. Ephron msuva mtaalamu wa maabara. alipotembelea zahanati ya Kilolo mapema asubuhi kwa lengo la kujionea mazingira ya zahanati hiyo. Akiwa hapo alikutana na Daktari mfawidhi Dkt. Selemani Jumbe
Mkuu wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Mhe. Asia Juma Abdallah






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...