Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akimuonesha Rais Dkt. John Pombe Magufuli sehemu ya Madawati yaliyotengenezwa na fedha zilizopatikana kutokana na kubana matumizi kutoka Ofisi ya Bunge katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amekaa kwenye moja ya Dawati katika hafla hiyo fupi ya ugawaji wa Madawati hayo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya Msingi Bunge George Samwel wakati akiangalia mfano wa darasa ya jinsi madawati hayo yatakavyo katika katika shule mbalimbali nchini.
Sehemu ya Wanafunzi wakiwa wamekalia kwenye madawati yatakayogawiwa leo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli , katika hafla ya ugawaji Madawati hayo, inayofanyika hivi sasa kwenye viwanja vya Karimjee, Jijini Dar es salaam.
Sehemu ya Madawati hayo yatakayowawiwa leo.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amezindua mpango wa ugawaji wa
madawati yanayotengenezwa kutokana na fedha zilizotolewa na Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania baada ya kubana matumizi katika bajeti yake.
Uzinduzi huo umefanyika
leo tarehe 13 Julai, 2016 katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es salaam
ambapo Rais Magufuli amekabidhi madawati 537 kwa mbunge wa jimbo la Ilala
Mheshimiwa Mussa Azan Zungu kwa niaba ya wabunge wa majimbo yote ya Tanzania
Bara na Tanzania Zanzibar ambayo yatagawiwa idadi hiyohiyo ya madawati kwa kila
jimbo.
Madawati hayo 537
ni sehemu ya madawati 61,385 ambayo yametengenezwa katika awamu ya kwanza na
yatafuatiwa na madawati mengine 60,000 yatakayogawiwa katika awamu ya pili na
yote kwa ujumla yatagharimu shilingi bilioni 4 ambazo zilitolewa na Bunge
tarehe 11 Aprili, 2016 baada ya kubana matumizi katika bajeti yake, ikiwa ni
kuitikia wito wa Mhe. Rais John Pombe Magufuli.
Mikoa
itakayonufaika katika awamu ya kwanza ya ugawaji wa madawati hayo ni Dar es
salaam, Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe,
Rukwa, Katavi, Unguja, Pemba na Tanga.
Akizungumza katika
hafla hiyo, Rais Magufuli amewashukuru na kuwapongeza wabunge kwa kutoa mchango
huo na pia amewapongeza wadau wengine ambao wameitikia wito wake wa kuchangia
madawati kwa lengo la kuondoa tatizo la wanafunzi kukaa chini.
Rais Magufuli
amesema baada ya kuanza kutekeleza ahadi ya kuondoa ada kwa shule za msingi na
sekondari, idadi ya wanafunzi waliojiandikisha kuanza darasa la kwanza
imeongezeka kutoka wanafunzi 1,282,100 hadi kufikia wanafunzi 1,896,584 sawa na
ongezeko la asilimia 84.5 hali iliyosababisha upungufu wa madawati 1,400,000
lakini tatizo hilo limetatuliwa kwa kiasi kikubwa ambapo mpaka sasa zaidi ya
madawati 1,000,000 yametengenezwa.
Aidha, Dkt.
Magufuli amelitaka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Jeshi la Magereza kuongeza
kasi katika utengenezaji wa madawati ili yakamilike haraka na kuanza kutumika.
Hafla hiyo
imehudhuriwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim
Majaliwa, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Tulia Ackson, Wabunge wa kamati ndogo ya tume ya huduma za bunge, Viongozi wa
Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Magereza pamoja na wanafunzi wa
shule ya msingi Bunge.
Gerson
Msigwa
Kaimu
Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es
salaam
13 Julai,
2016
Orodha ya Mgawanyo wa Madawati hayo.








M/Mungu akujaalieMheshimiwa Rais pamoja na watendaji waongofu katika hili la madawati. Tulikuwa tunaona na wengine tumepitia katika kukaa juu ya vipande vya mawe na kukaa chni kabisa katika Mashule yetu. Tulikuwa tukijiuliza hivi tumemkosea nini Mwenyezi Mungu? Kumbe ilikuwa ni makusudi ya baadhi ya waliopewa dhamana ya kutuongoza. MwenyeziMungu akuongoze katikamkutuletea neema na maendeleo katika nchi yetu adhimu.Mimi binafsi nakutakia maisha mema na marefu na uendelee kufanya kazi zako kwa bidii ukiwa na wafanaykazi wengine mahiri.Asante Serikali, Asante Mungu
ReplyDeleteHuu ndo uzuri wa kuwa na raisi mwalimu na msomi kwani anajali elimu. Pia anaamini elimu ni applicable ndo maana hukagua vyetu vya maafisa wake. wale waliokuwa wamezoea msemo wa "kufeli masomo siyo kufeli masiha" watapumzika kwa miaka 10 hivi kwanza. Maanake ilishazoeleka kilaza wako unamkuta kwenye interview pannel ya interviewers pale uombapo kazi. Hiyo ilivunja moyo wa watoto kusoma wakiamini masomo hayana kitu bali zali.
ReplyDeleteFatiki za Jkt...
ReplyDeleteHili ni jambo zuri ninawapongea lakini ningependekeza Fikeni vijiji kabisa jamani kulea wazazi hawajiweji hata kuchangia! sasa Bunge si hata mzazi moja tu au wawili wanaweza kuchangia hayo madawati! Nendeni kula ambako hakufikiki~
ReplyDelete