Timu ya Mpira wa Miguu Ufukweni ya Tanzania imepangwa kucheza na Ivory Coast kati ya Agosti 26, 27 au 28, 2016 kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2017 zitakazofanyika Lagos, Nigeria. Mchezo wa marudiano unatarajiwa kufanyika kati ya Septemba 16, 17, au 18.

Fainali za Mpira wa Miguu Ufukweni ambazo zitafahamika pia kama 2016 CAF Beach Soccer Championship, zitafanyika kuanzia Desemba 13 hadi 18, 2016 jijini Lagos, Nigeria kwa kushirikisha timu nane.

Tayari Nigeria imepasishwa kuwa mshiriki kwa sifa ya uenyeji waketi timu nyingine 14 zinawania kucheza fainali hizo. Timu nyingine zinazowania ni

Cape Verde v Senegal
Uganda v Misri
Liberia v Morocco
Kenya v Ghana  
Msumbiji v Madagascar  
Sudan v Libya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...