Ni Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Ibaga,tarafa ya Kirumi,wilayani Mkalama wakiwa kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mbunge wa jimbo la Iramba Mashariki,Bwana Allan Kiulla kwa lengo la kufanya mrejesho wa maamuzi mbalimbali waliyopitisha katika kikao cha Bunge lililomalizika mwezi uliopita.
 Ni Mbunge wa jimbo la Iramba Mashariki,Bwana Allan Kiulla akisaini kitabu cha wageni katika Kijiji cha Ibaga mara tu baada ya kuwasili katika uwanja wa mkutano wa Kijiji hicho.
Ni Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Ibaga,wakiwemo wanawake na wanaume wakimsikiliza Mbunge wa jimbo la Iramba Mashariki,Bwana Allan Kiulla

Na Jumbe Ismailly,Mkalama.
ZAIDI ya ekari 250 za mazao mbali mbali yakiwemo mahindi,mtama,karanga na alzeti katika kata ya Ibaga,tarafa ya Kirumi,wilayani Mkalama yameharibiwa na wanyama waharibifu waitwao ngedere na hivyo kusababisha wakulima wengi kutofikia malengo waliyojiwekea ya mavuno yao waliyotarajia.

Ngedere hao wanaokadiriwa kufikia zaidi ya 20,000 wamekuwepo katika kata ya Ibaga,tarafa ya Kirumi,Wilayani Mkalama na kuendelea kuwasumbua wakulima wa mazao hayo kwa kipindi cha takribani kati ya miaka saba hadi minane sasa.

Akitoa ufafanuzi wa swali lililoulizwa kwa Mbunge wa jimbo la Iramba Mashariki,Allan Kiulla na mkulima wa Kijiji cha Ibaga,Mwendomgelwa Kingu aliyetaka kufafamu serikali imejipangaje kuondoa kero ya wanyama hao waharibifu,diwani wa kata ya Ibaga,Salumu Abdallah Lindi alibainisha kuwa kero hiyo inatokana na Halmashauri ya wilaya ya Mkalama kutokuwa na wataalamu wa idara ya wanyamapori wa kupambana na wanyama hao waharibifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 13, 2016

    Mpelekeeni Magembe yeye anaita tumbili wekundu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 14, 2016

    Hii habari inanikumbusha kitabu cha shule ya msingi nadhani darasa la tatu enzi hizo. "Twende tukaweinde"

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...