Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii.

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini mwenye makazi yake Mkoani Morogoro, Francis Cheka ameondoka mjini humo kwenda Dar es Salaam kuitikia wito wa Polisi.

Cheka ambaye alijisalimisha katika kituo cha Polisi Morogoro baada ya kupokea wito wa kufika kituoni kufuatia kupata barua ya wito huo.
"Nimefika kituoni na kuelezwa kuwa nimefunguliwa mashtaka ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa Promota Siraju Kaike  hivyo nimefika hapo na kujidhamini na kuamua kwenda kituo cha Polisi Osterbay kwa ajili ya kutoa maelezo" amesema Cheka.

Amesema kuwa mashabiki wake wawe na imani nae kwani huo sio utapeli kama unavyozungumzwa bali ni mapromota uchwara wanataka kula migongoni mwa mabondia.

"Lazima nikwambie ndugu mwandishi Mimi nishakuwa mkubwa sasa na hizi ngumi zinauma hivyo Biashara ya pesa baadae ilishapitwa na wakati" alisema Chema.

Hivyo tuombe mungu mambo yote yatajulikana mahakamani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...