Sakata la mchezaji Zahoro Pazi aliyesajiliwa na timu ya Mbeya City limefikia tamati leo baada ya FC Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutuma hati yake ya uhamisho wa kimataifa (ITC) kwenda katika shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF).
Mbeya City walishindwa kumtumia mchezaji huyo ingawa ni mtanzania kwa kuwa hakuwa na hati ya uhamisho kutoka katika timu yake ya awali kuchelewesha kumtumia kwa mchezaji huyo.
Zahoro aliyesajiliwa katika dirisha dogo la usajili kwa sasa anaweza kuitumikia klabu yake hiyo mpya ya Jijini Mbeya baada ya ITC yake kuwasili TFF
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...