Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.
Mbunge wa jimbo la Kigamboni Dk Faustine Ndugule amemuomba Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa kuangalia upya tozo za daladala zinazo pita katika daraja la kigamboni ili kutoa unafuu kwa wananchi waishio Kigamboni kama ilivyokuwa madhumuni ya kujengwa kwa daraja hilo.
Akizungmza na globu ya jamii Dk Ndugulile amesema kuwa wananchi wamekuwa watumwa kwa usafiri kwa miaka mingi huku wakitegemea daraja liwe mkombozi wao, lakini sasa imekuwa kinyume kutokana na gharama za kupita kwa daladala katika daraja hilo.
“gari moja yaani daladala linatakiwa kulipa shilingi 5000 kwa kila trip,jambo ambalo ni gharama kuliko biashara yenyewe ambayo ni huduma kwa wanachi hivyo kwa hesabu za haraka kama dereva atafanya trip 10 atatakiwa kulipa shilingi 50,000/- kitu hicho kinawawia vigumu kufanya kwa madereva wa daladala” amesema Dk Ndugulile.
Amesema kuwa amefanya jitihada za kila namna kwa kuzungumza na mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF ambo wao ndio wanaendesha daraja hilo kwa kuwaandikia barua rasmi hili waweze kupunguza tozo hizo kwa ajili ya daladala lakini bado aoni dalili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...