![]() |
Kijana aliye patikana na hatia ni Natdanai Khongdee (Umri, Miaka 19, pichani juu wa pili kulia) ambapo mkuu wa polisi wa Nchi hiyo Chakthip Chaijinda, (wa tatu kushoto) alimtangaza mbele ya vyombo vya habari vya Nchi hiyo. ----------------------------------------------------------------------------- |
Na Yusuph Kileo
Mswada wa sheria mtandao nchini Thailand uliwekwa mezani kujadiliwa takriban wiki kadhaa zilizo pita. Muswada huo ambao ulikua ukingoja kupitishwa kuwa sheria umepelekea kelele nyingi nchini humo ambapo wananchi wake walitaka ufanyiwe marekebisho kabla ya kuwa sheria huku wengine wakiukataa kabisa.
Mswada wa sheria mtandao nchini Thailand uliwekwa mezani kujadiliwa takriban wiki kadhaa zilizo pita. Muswada huo ambao ulikua ukingoja kupitishwa kuwa sheria umepelekea kelele nyingi nchini humo ambapo wananchi wake walitaka ufanyiwe marekebisho kabla ya kuwa sheria huku wengine wakiukataa kabisa.
Wana usalama mtandao nchini humo
walijaribu kutoa ufafanuzi ambao haukuzaa matunda na hatimaye kutaka msaada
kutoka kwa wanausalama mtandao wa maeneo mengine.
Wiki mbili zilizo pita wahalifu
mtandao Nchini humo walitangaza kushambulia tovuti za serikali ili
kushinikiza mamlaka kufanyia kazi marekebisho ya sheria hizo za mtandao ambazo
walidai hawakukubaliana nazo – Baadae walianza kushambulia tovuti mbali mbali
na kusababisha mtafaruku mkubwa.
Tovuti ya polisi ya nchini humo
(Royal Thai Police Office) ni miongoni mwa tovuti zilizoshambuliwa kimtandao
ambapo ilidukuliwa na baadae kuangushwa kabisa. Kitu ambacho kilipelekea hasira
kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hiyo.
Naibu waziri mkuu na waziri wa
ulinzi Mh. Prawit Wongsuwon, alitangaza kukamata washukiwa tisa (9) wa uhalifu
huo mtandao pamoja na vifaa vyao huku akiongeza kuwa serikali ya nchi hiyo haitalinyamazia
tukio hilo na kusema watachukua hatua stahiki kwa kila atakaethibitika na
uhalifu huo.
Tayari kati ya tisa (9) waliokamatwa
, Kijana mdogo mmoja amepatikana na hatia huku wengine nane (8) bado
wanaendelea kufanyiwa uchunguzi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...