Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Kiungo wa zamani wa Real Madrid, Arsenal na Monaco Emmanuel Adebayor anatajwa kuwa muda wowote kuanzia sasa atajiunga na klabu ya Yanga ya  Dar es salaam kwa mkataba mnono.

Taarifa zilizotufikia zinamtaja nahodha huyo wa timu ya Taifa ya Togo kuwa atajiunga na timu hiyo hili waweze kutetea ubingwa na kujiandaa na michuano ya kimataifa ya klabu bingwa Afrika.


Adebayor anataka kujiunga na wana-Jangwani hao ikiwa ni siku chache baada ya timu yao ya Taifa ya Togo kutolewa katika michuano ya AFCON.
Adebayor kama atajiunga klabu hiyo ya Yanga atakuwa mchezaji wa kwanza kutoka ligi ya mabingwa ulaya kuja kucheza katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...