LakeFmHabari.

Baadhi ya akina mama waliojifungulia katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mwanza Sekou Toure, wameishukuru serikali pamoja na wadau wengine wa afya kwa kuendelea kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo.

Akina mama hao wameyasema hayo jana baada ya mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Mapinduzi mkoani Mwanza, kukabidhi msaada wa vitanda, magodoro, mashuka na vyandarua katika hospitali hiyo.

Wamesema hivi sasa huduma za afya hususani kwa mama na mtoto zimeboreshwa katika hospitali hiyo ikilinganishwa na kipindi kilichopita ambapo wameomba maboresho zaidi yaendelelee ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya.

Mganga Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonard Subi amesema huduma za afya zinaendelea kuboreshwa katika halmashauri mbalimbali mkoani Mwanza huku msisitizo ukiwa ni kuwahamasisha akina mama kujifungulia kwenye vituo vya afya.

Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Mapinduzi mkoani Mwanza, Kemirembe Lwota kwa kushirikiana na taasisi ya Mo Dewji amesaidia upatikanaji wa mashuka 100 pamoja na vitanda 20 vilivyoambana na magodoro pamoja na vyandarua.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza, mbunge viti maalumu CCM Mkoani Mwanza, Mkuu wa Mo Dewji Foundation, Mwenyekiti wa UWT mkoani Mwanza pamoja na wadau wengine, wakiwa kwenye wodi ya akina mama hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mwanza, kujionea hali ya wodi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...