LakeFmHabari.
Baadhi
ya akina mama waliojifungulia katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa
Mwanza Sekou Toure, wameishukuru serikali pamoja na wadau wengine wa
afya kwa kuendelea kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo.
Akina
mama hao wameyasema hayo jana baada ya mbunge wa viti maalumu kupitia
Chama cha Mapinduzi mkoani Mwanza, kukabidhi msaada wa vitanda,
magodoro, mashuka na vyandarua katika hospitali hiyo.
Wamesema
hivi sasa huduma za afya hususani kwa mama na mtoto zimeboreshwa katika
hospitali hiyo ikilinganishwa na kipindi kilichopita ambapo wameomba
maboresho zaidi yaendelelee ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma
bora za afya.
Mganga
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonard Subi amesema huduma za afya
zinaendelea kuboreshwa katika halmashauri mbalimbali mkoani Mwanza huku
msisitizo ukiwa ni kuwahamasisha akina mama kujifungulia kwenye vituo
vya afya.
Mbunge
wa viti maalumu kupitia Chama cha Mapinduzi mkoani Mwanza, Kemirembe
Lwota kwa kushirikiana na taasisi ya Mo Dewji amesaidia upatikanaji wa
mashuka 100 pamoja na vitanda 20 vilivyoambana na magodoro pamoja na
vyandarua.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza, mbunge viti maalumu CCM Mkoani Mwanza, Mkuu wa Mo Dewji Foundation, Mwenyekiti wa UWT mkoani Mwanza pamoja na wadau wengine, wakiwa kwenye wodi ya akina mama hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mwanza, kujionea hali ya wodi hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...