Benki ya Exim Tanzania hivi karibuni ilitunukiwa tuzo mbili katika hafla iliyoandaliwa na Shirikisho la Waajiri Tanzania (ATE). Benki ya Exim ilishinda tuzo ya Uongozi na Utawala- Rasilimali Watu (HR- Leadership & Governance) na tuzo ya Ushirikisho wa Wafanyakazi (Employee engagement). Tuzo hizo mbili muhimu zilitolewa kwa benki katika hafla ya mfanyakazi bora wa mwaka 2016 na zilikabidhiwa na Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi.

Utawala bora katika kitengo cha rasilimali watu na ushirikishwaji wa wafanyakazi ni nguzo muhimu katika uendeshaji wa kitengo hicho cha Exim ambacho hufanya kazi ya kuhakikisha wafanyakazi wanatekeleza majukumu yao katika namna ambayo inayohakikisha benki inafanikisha mipango na malengo yake huku ikiendelea kupata faida kila mwaka. Mwaka 2016 Exim ilitimiza miaka 19 ya operesheni huku ikifanya bidii katika kuongeza viwango vya kushirikisha wafanyakazi wake katika shirika hilo.

Benki ilifanya vizuri sana katika kuhamasisha utawala bora na ushirikishwaji wafanyakazi kupitia njia nyingi za asili. Benki ilipitia upya sera ya rasilimali watu na kuongeza vifungu vinavyohamasisha wafanyakazi kuwa na maisha yenye afya bora. Benki iliingia katika mchakato wa kuimarisha mfumo wa kufanya tathmini ya utendaji ambao ni wa kisasa na umeunganishwa katika mfumo ulioko mtandaoni unaoitwa Adrenalin ambao ni wa uwazi sana.

Katika uajiri mkakati mkuu ulikuwa ni kuhakikisha usawa wa  jinsia katika wafanyakazi wa kike na kume ambao jumla yao wanafikia 1000. Benki inahakikisha kuwa wafanyakazi watendaji bora wanatambuliwa kupitia tuzo za wafanyakazi, tuzo za wafanyakazi wa muda mrefu, kupandishwa vyeo kutoka nafasi za chini kwenda kwenye nafasi za kati hadi nafasi za juu za umeneja katika shirika kupitia matangazo ya nafasi za kazi ya ndani na programu ya uwezo inayoitwa HIPO. Benki pia iliboresha miundo ya vitengo vyake vyote, kuboresha vyeo na kufanya tathmini za ajira ambazo ziliboresha mifumo ya kazi na hivyo kusababisha usimamizi mzuri na uzalishaji katika vitengo. Vilevile benki iliboresha mifumo ya mawasiliano kupitia majukwaa ya majadiliaano kati ya menejimenti na wafanyakazi ili kujadili utendaji wa benki na kupeana mrejesho uliolenga kuimarisha utendaji wa benki.  

Kwa upange mwingine benki ya Exim imekuwa ikitumia teknolojia ili kuwapatia wafanyakazi zana bora za kuongeza uzalishaji, kuboresha huduma kwa wateja na mafunzo na maendeleo. Benki ilijikita katika miradi kadhaa iliyolenga kutekeleza teknolojia mbalimbali katika utendaji kwa kuweka namba maalum “whistleblower” inayoweza kutumika na wafanyakazi na wateja pia kutoa taarifa za kiutendaji za benki ikiweka benki katika jukwaa la kidijitali zaidi.

Katika mafunzo na maendeleo, benki ilianzisha mfumo wa kujifunza kupitia mtandao unaoitwa Elimika. Kusudi la Elimika ni kutoa maarifa kwa wafanyakazi kwa kuwapatia ujuzi unaohitajika katika utendaji wa kazi zao. Matokeo ya Elimika ni wafanyakazi walioelimika zaidi, wenye uelewa na ushirika zaidi. Kasi ya mageuzi haya imekuwa kubwa na kuleta ukuaji katika biashara nchini Tanzania na kuwezesha wafanyakazi walio makao makuu kuweza kutoa msaada na ushirikiano kwa wengine mikoani na katika kampuni tanzu.

“Exim inajivunia kuwa benki ambayo inajikita katika uvumbuzi na teknolojia. Tunatumia suluhisho za teknolojia ili kutengeneza mazingira yanayoboresha kwa kiwango kikubwa uwezo wa wafanyakazi. Kozi hizi zinasaidia wafanyakazi kuwa na uelewa mkubwa wa majukumu yao na pia kuwa na zana za vitendo kuendeleza ujuzi na vipaji vyao,” alisema Fredrick Kanga ambaye ni mkuu wa kitengo cha rasilimali watu cha Exim.

“Ni matumaini yetu kuwa wafanyakazi wetu wataendelea kujenga ujuzi wao kupitia Elimika. Na menejimenti ya Exim itaendelea kuboresha mifumo yake ili tuendelee kuwa mwaajiri bora kabisa nchini. Nina imani kubwa kuwa tuna uwezo huo na tumeamua kuileta Exim katika kiwango hicho mwaka huu,” alimalizia Fredrick Kanga. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...