Mjumbe wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi inayoshughulikia masuala ya Viongozi Wakuu wa Kitaifa Simai Mohamed Said (wa pili kulia) alipokuwa akitoa mchango wake wakati wa mazungumzo na Uongozi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi wakati Ujumbe wa Kamati hiyo walipotembelea Ofisi hapo Ikulu Mjini Unguja leo kuzungumzia utekelezaji wa masuala mbali mbali yanayohusu Ofisi hiyo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi inayoshulikia masuala ya Viongozi Wakuu wa Kitaifa Omar Seif Abeid akitoa maelekezo wa Watendaji wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi leo wakati ujumbe wa Kamati hiyo ulipokutana na watendaji hao ikulu Mjini Unguja kuzungumzia masuala mbali mbali ya kiutekelezaji (kushoto) Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Nd. Salum Mauli Salum.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...