Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Leonard Chamriho akitoa salamu kwa niaba ya serikali wakati wakati wa kuaga mwili wa Rubani na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) marehemu Kenan Mhaiki Rubani wakati wa shughuli ya kuaga mwili wake iliyofanyika nyumbani kwake Kunduchi jijini Dar es Salaam Januari 2 2017. Mwili wa marehemu umesafirishwa jana kwenda Songea mjini mkoani Ruvuma kwa mazishi yanayotayarajiwa kufanyika leo Januari 4, 2017 kwenye Makaburi ya Matogoro.
Waombolezaji wakimpa mkono wa pole kaka wa marehemu Bw. Oliver Mhaiki
Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Balozi Ombeni Sefue akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Kenani Mhaiki Rubani Mstaafu wa ndege za marais wa Tanzania wakati wa shughuli ya kuaga mwili wake iliyofanyika Kunduchi, jijini Dar es Salaam jana. Mwili wa marehemu umesafirishwa jana kwenda Mkoani Ruvuma kwa mazishi yanayotayarajiwa kufanyika Januari 4 2017. Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akitoa heshima zake za mwisho Picha na Robert Okanda. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA |
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...