BENDI MPYA
•Tarehe 26-Feb-2016, bendi mpya ya BMM ilizinduliwa rasmi katika ukumbi wa Mzalendo Pub. Bendi hiyo, pamoja na wanamuziki wengine, inaundwa na Mule Mule FBI (Rais wa bendi) na Totoo Ze Bingwa. Bendi pia inamjumuisha mpiga solo mahiri Losso Mukenga, ambaye pia ni mpiga solo wa Ally Kiba. Hata hivyo bendi hii ilidumu kwa muda mchache sana.
•Tarehe 08-Apr-2016 (Ijumaa), bendi mpya ya Sky Melodies chini ya uongozi wa Nicco Millimo, ilitambulishwa ndani ya Club la Aziz Classic, Dodoma.
•May-2016, bendi mpya ya Ivory Band ilianzishwa. Bendi hii kwa asilimia kubwa imeanzishwa na wanamuziki waliotokea bendi ya Double M Plus baada ya kutokea mtafaruku. Wanamuziki hawa ni kama Dogo Rama, Saleh Kupaza, Jojo Jumanne, Rashid Sumuni na kadhalika.
•Nov-2016, bendi ya Original Dar Musica ilianzishwa chini ya mwanamuziki Jaddo Field Force. Hii ni baada ya mwanamuziki Jaddo Field Force kuenguliwa (au kujiengua) katika bendi ya Dar Musica.
•Tarehe 24-Dec-2016 (Jumamosi), bendi mpya inayoitwa DSS Band (Dar-es-Salaam Super Sound) “Wazee wa Kujilipua” yazinduliwa rasmi katika ukumbi wa Family Bar, Tabata Mbuyuni. Bendi hiyo inamilikiwa na wanamuziki Ferguson na Rogart Hegga “Caterpillar”.
BOFYA HAPA KUONA MATUKIO ZAIDI
BOFYA HAPA KUONA MATUKIO ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...