Waziri wa mazingira katika Serikali ya Burundi, Emmanuel Niyonkuru, amefariki dunia baada ya kupigwa risasi mjini Bujumbura saa chache tu baada ya kuingia mwaka mpya.
Polisi nchini wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa kusema amepigwa risasi alipokuwa akielekea nyumbani kwake eneo la Rohero.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, ameapa kuchukua hatua kali za kisheria kwa atakayepatikana na hatia ya kuhusika katika mauaji hayo.
Mamia ya watu , wakiwemo maafisa wa ngazi za juu katika jeshi wameuawa tangu Rais Pierre Nkurunziza kuwania urais kwa muhula wa tatu 2015, hatua ambayo wapinzani wanasema ni kinyume na sheria.
Lakini hii ni mara ya kwanza kwa waziri wa serikali kuuawa.
Kwa miezi kadhaa taifa hilo limekuwa tulivu.CHANZO:BBC SWAHILI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...