Mbunge wa Jimbo la Nkenge Balozi Dr. Diodorus Buberwa Kamala (mwenye miwani) akizungumza na mwananchi wa kata Mabale aliyefika kuchota maji katika bwawa la maji la Akashwa lililo kata Mabale. Bwawa hilo limekauka kwa kiasi kikubwa kutokana na kukosekana mvua kwa muda mrefu. Balozi Kamala ametembelea pia mabwaya ya Nyankere na Lwoga ambayo yako hatarini kukauka kama mvua hazitanyesha ndani ya kipindi kifupi kijacho.
Mkazi wa Kata Kilimilile akichota maji baada ya mradi wa kata Kilimilile kuanza kutoa maji. Mbunge wa Jimbo la Nkenge Balozi Dr. Diodorus Buberwa Kamala ameshuhudia kuanza kazi kwa mradi huo na amewaomba wananchi kutunza mradi huo. Balozi Kamala anaendelea na ziara ya kukagua miradi ya maji Wilayani Missenyi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...