Nasieku
Kisambu Mkurugenzi wa Mipango Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA)
akizungumza katika mafunzo ya Haki za Wanawake na Jinsi ya kufanya
utetezi katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa yakiwa na lengo
la kuongeza uelewa wa misingi ya kulinda na kutetea haki za wanawake na
watoto Kitaifa , Kikanda na Kimataifa.
Kuelewa
mifano iliyopo katika Kanda, Kikanda na kimataifa inayolinda haki za
wanawake , Haya ni mafunzo yanayolenga kujenga uwezo wa Taasisi
zinazotetea haki za wanawake kutumia fursa zilizopo katika mikataba,
Taasisi na mifumo ili kuweza kubadilisha sera na sheria kandamizi na
kutetea haki za wanawake.
Mafunzo
hayo yanayofanyika kwenye hoteli ya Courtyard Upanga jijini Dar es
salaam yameandaliwa na Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) na
kwa ushirikiano na mashirika mengine yanayotetea haki za wanawake na
watoto ambapo wadau mbalimbali kutoka katika taasisi hizo wameshiriki
katika mafunzo hayo
Maria
Matui Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake Wanasheria Tanzania
(TAWLA) akifungua mafunzo hayo ya siku mbili yanayofanyika kwenye hoteli
ya Courtyard Upanga jijini Dar es salaam.
Mkufunzi
wa Mafunzo hayo Dk. Clemence Mashamba akitoa mada wakati wa mafunzo
hayo yanayoendelea kwenye hoteli ya Courtyard Upanga jijini Dar es
salaam.
Washiriki wa Mafunzo hayo wakiwa katika picha ya pamoja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...