NA VICTOR MASANGU, KIBITI
LICHA ya serikali ya awamu ya tano kuongeza juhudi za kuboresha sekta ya afya katika maeneo mbali mbali hapa nchini bado sehemu nyingine utoaji wa huduma hali bado ni tete kutokana na kukabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ukosefu wa wauguzi,madaktari, madawa, magari ya kubebea wagonjwa,vitanda pamoja na vifaa tiba hivyo kusababisha wagonjwa kupata shida kubwa pindi wanapokwenda kupatiwa matibabu.
Changamoto hizo ambazo zinadaiwa ni sugu na hazijafanyiwa utekelezaji wowote zimeweza kubainika baada ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Japo kufanya ziara yake ya kikaz ya siku mbili kwa wananchi wa Wilaya ya Kibiti Mkoa wa Pwani hususan katika maeneo ya wananchi wanaoishi katika maeneo ya Delta kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo pamoja na kubaini changamoto za muda mrefu zilizokuwa zinawakabili ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi.
Naibu Wazari Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo wa kati kati akiwa kwenye boti katika ziara yake ya kikazi katika Wilaya ya Kibiti na viongozi wengine wa serikali,na wa kwanza kulia kwake ni Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Khatibu Chaurembo kwa ajili ya safari ya kwenda kuwatembelea wananchi wa maeneo ya Delta kwa ajili ya kukagua miradi ya mbali mbali maendeleo.(PICHA NA VICTOR MASANGU) Taarifa kamili BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...