Na Judith Mhina - MAELEZO
Waziri
katika Serikali ya Awamu ya Kwanza, Pili na ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Mtaalamu wa lugha ya Kiswahili, Dkt Mohammed Seif Khatibu (pichani) amesema
Mapinduzi ya Zanzubar ya mwaka 1964 yalimaliza mateso ya muda mrefu
waliyoyapata Waafrika wa Tanzania Bara na Visiwani.
Dkt. Mohammed Seif Khatibu amesema hayo alipohojiwa na Idara ya Habari - MAELEZO leo
kuhusiana na mafanikio yaliyopatikana tangu mapinduzi ya Zanzibar yalipofanyika
miaka 53 iliyopita.
Amesema, Mapinduzi yameondoa madhila ya utumwa, masuria, kubaguliwa,
kufanyishwa kazi, kudhalilishwa, kunyanyaswa, kudharauliwa na kuuzwa kama
samaki:
“Inashangaza
kuona Watanzania hawasheherekei ipasavyo Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwa kama si
Mapinduzi hayo mateso na madhila kwa Waafrika wa Bara na Visiwani yangeendelea”.
“Madhila ya Zanzibar hayawagusi Waafrika wa Zanzibar peke yake, bali pia
Waafrika wa Tanzania Bara”. Kusoma zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...