Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais, Dkt. John
Pombe Magufuli mara tu ilipoingia madarakani mwezi Oktoba mwaka juzi ilitoa
vipaombele vyake kadhaa vya kutelezwa na wizara zake mbalimbali huku Wizara ya
Maliasili na Utalii ikikabidhiwa majukumu mazito matatu ya kutekeleza katika
kipindi cha uongozi wake.
Majukumu hayo yaliyotolewa na Rais Magufuli
wakati wa hotuba yake ya kwanza ya kulihutubia bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania mjini Dodoma, ni yale ya kuhakikisha kuwa wizara hiyo inakomesha
vitendo vya ujangili, kuongeza mapato ya serikali na kushuulikia utatuzi wa
migogoro ya mipaka kwenye maeneo ya hifadhi nchini.
Wizara
ya Maliasili na Utalii, imesema kuwa imejipanga kuhakikisha kuwa malengo yake
ya uhifadhi wa Maliasili, Malikale na Kuendeleza Utalii pamoja na utekelezaji
wa vipaombele ilivyopewa na Serikali ya awamu ya tano kuwezesha kufikia malengo
hayo yanatimia kwa wakati.
Kwa upande wa utatauzi wa migogoro kwenye maeneo ya hifadhi
nchini, Wizara hiyo imejipanga kuwashirikisha wadau wote wanaohusika na
migogoro hiyo kwa kukaa nao pamoja kwenye vikao vya majadiliano na kuweka
mikakati ya pamoja ya kufikia suluhu ya migogoro hiyo kwa faida ya Serikali na
wadau wote wanaohusika.
Hivi karibuni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi
Ramo Makani alifanya ziara ya kiutafiti katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na
Pori Tengefu la Liliondo, lengo kuu la ziara hiyo ikiwa ni kuona uhalisia wa
changamoto zilizopo pamoja na kupata taarifa sahihi kutoka kwa wadau husika,
alifanya hivyo bila ya kujitambulisha kwa lengo la kupata taarifa sahihi
kuhusiana na migogoro hiyo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (wa pili kushoto) akioneshwa Ramani ya Kijiji cha Ololosokwan na Diwani wa Kata hiyo, Yanick Ndoinyo alipotembelea kijiji hicho hivi karibuni kuona changamoto za uhifadhi. Kulia ni Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji cha Ololosokwan, Emmanuel Salteimoi.
Kundi la mifugo likiwa ndani ya Pori Tengefu la Loliondo, karibu kabisa na mpaka wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kulia) akizungumza katika kikao cha wadau wa mgogoro wa Pori Tengefu la Loliondo alichokiitisha katika ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Tarafa ya Loliondo mkoani Arusha hivi karibuni.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...