Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akijibu maswali yaliyoulizwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakati wa ziara ya kikazi iliyofanyika leo jijini Mbeya.Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Kanali Mstaafu Masoud Ally.( Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
 Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kapteni Mstaafu Goerge Mkuchika, akizungumza wakati wa kipindi cha kuuliza maswali yaliyoelekezwa kwa Idara zilizopo ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.Kamati hiyo imekutana  jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
 Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Juliana Shonza (katikati) akizungumza wakati wa kipindi cha kuuliza maswali yaliyoelekezwa kwa Idara zilizopo ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi .Wengine ni wajumbe wa kamati hiyo.Kamati hiyo ya Bunge  iko jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
 Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Rehema Madusa akizungumza wakati wa mkutano na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama,iliyokutana jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
 Mkuu wa Idara ya Uhamiaji mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi , Asumsio Achachaa, akijibu maswali yaliyoelekezwa kwenye Idara yake na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama(hawapo pichani), wakati wa mkutano na kamati hiyo iliyokutana Jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Jeshi la Magereza mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi(ACP)  Paul Kajida, akijibu maswali yaliyoelekezwa kwenye Idara yake na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama(hawapo pichani),  wakati wa mkutano na kamati hiyo iliyokutana  Jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...