Serikali ya Manispaa ya wilaya ya Temekee na kampuni ya Ujenzi ya China CRJE  wametiliana saini mkataba wa Ujenzi wa Daraja litakalo unganisha  eneo la kijichi na Tuangoma  wilayani humo.

Akizungumza katika hafla hiyo mwakilishi wa Mkuu wa wilaya ya Temeke   ambaye pia ni katibu tawala  Wilaya hiyo Hashim Komba  , amesema daraja hilo linajengwa ili kuondo usumbufu wanaoupata  wananchi wanaoishi  maeneo hayo kwa kuzunguka Kigamboni na kongowe wakati wa masika.

Aidha afafanua kuwa Daraja hilo litakuwa na urefu wa Mita 800 na barabara za mitaa zaidi ya kumi zenye urefu wa Kilomita 1.8   na  barabara  nyingine zenye urefu wa kilomita 84 zote zitajengwa kwa kiwango cha lami na kitapimwa viwanja zaidi ya mianane kuzunguka eneo  la mradi huo.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Ujenzi CRJE Zhao Yefang ameshukuru kupewa kazi hiyo ana ameahidi kufanya kwa viwango kama walivyo jenga Daraja la Kigamboni watahakikisha ubora na thamani ya hela vinazingatiwa na ndani ya mwaka mmoja watakabidhi Daraja hilo.
Wakisaini Mkataba katikati ni Mstahiki Meya Wa Manispaa ya Ilala Bw Abadallah Chaulembo,Kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw Nassib Mbaga na Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Ujenzi CRJE Bw Zhao Yefang
  Katibu mkuu wa Wilaya ya Temeke Bw Hashim Komba akiongea na Wananchi wa Kijichi kuhusu swala zima la Utengenezwaji wa Daraja hilo ili kuondoa Usumbufu wanaoupata wananchi kuzunguka Kigamboni na Kongowe wakati wa Msimu wa Masika.
Mstahiki Meya wa Temeke Bw Abdallah Chaulembo akizungumza na wananchi wa Kijichi kuhusu ujenzi wa Daraja unaotarajia kuanza mapema Mwaka huu katika Eneo hilo
Baadhi ya Wananchi wa Kijichi wakiwa Katika Mkutano huo.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...