
Na Rhoda Ezekiel Kigoma.
MKUU wa Mkoa wa Kigoma , Brigedia Jenerali msaafu Emanuel Maganga amewataka Wananchi wa Mkoa wa Kigoma kuacha tabia ya kudai fidia mara mbili katika maeneo yao yanayo chukuliwa kwaajili ya kufanyiwa uwekezaji wa viwanda na uchumi hali inayopelekea Mkoa huo kushindwa kuendelea kwasababu ya Baadhi ya watu wanaong'ang'ania maeneo kwa kudai walipwe fidia ya ziada.
Rai hiyo aliitoa jana wakati akitoa salamu za Mwaka mpya kwa Wananchi wa Mkoa huo katika kanisa la Kiinjili la kiruthel Tanzania KKKT ushirika wa Kigoma alisema Mkoa wa kigoma kwa mwaka 2017 tumeandaa kubolesha Uchumi kwa kuanzisha viwanda vingi na kutenga maeneo kwaajili ya Shughuli za kiuchumi jambo ambalo litasaidia mkoa huu kufunguka kiuchumi.
Maganga alisema kumekuwa na tabia ya Wananchi wengi wa Mkoa wa huu kudai fidia mara mbili unakuta eneo moja wanakuja watu zaidi ya wawili kudai fidia ya sehemu moja hali inayo pelekea Serikali kushindwa kufikia malengo yake kwakuwa fedha inayotengwa kwaajili ya suala la kuwekeza kwenye uchumi inaishia kuwalipa watu fidia tumeyaona hayo wakati wa kulipa fidia kwa eneo tunalo tarajia kujenga Bandari ya Nchi kavu.
"Serikali ya Mkoa wa Kigoma kwa mwaka uliopita tumejitahidi sana kubolesha huduma za Kijami ikiwa ni pamoja na elimu ambayo imetuletea matokeo mazuri kwa mwaka uliopita Mkoa wa Kigoma umeshika nafasi ya kwanza kitaifa na umeongoza kwa asilimia 94% kwa mwaka huu kipaumbele chetu ni kuhakikisha tunakuza uchumi wa Mkoa wetu,"alisema Maganga.
Alisema kuanzia sasa utaandaliwa utaratibu utakao saidia kujua ninani anastahili kulipwa fidia na kila eneo moja atalipwa Mtu mmoja watu wasitumie Fulsa ya uwekezaji wa Serikali kama njia ya kutajilika na kupatia mitaji tutajitahidi kufanya kazi hii kwa ufanisi ilikuhakikisha malengo tuliyo yaweka kwa mwaka huu yanakamilika.
Aidha Maganga amewaomba Wananchi kufanya kazi kwa bidii na kuwaahidi huduma zote zitakazo tolewa na Serikali yake zitakuwa nzuri na zenye lengo la kuwasaidia wananchi wenye kipato cha chini iliwaweze kuinuka na kufikia uchumi wa kati kwa kubolesha miundombini mbalimbali ya kijamii itakayo fungua Fulsa za maendeleo ya Mkoa huo.
Aliwaomba wafanya biashara kusafilisha bidhaa mbalimbali kupeleka nje ya Mkoa wa Kigoma kwa kutumia barabara zilizo jengwa vizuri kwa mwaka huu ilikuhakikisha Uchumi wa Mkoa wa Kigoma unakuwa kwa kasi na kwa kiwango cha juu.
Nae Mchungaji wa Ushirika wa kanisa la Kiinjili la Kiruthali Mkoa wa Kigoma Emanuel Mtoi aliiomba serikali kuwahurumia Wanachi kwa kuwaboleshea huduma za kufanyia biashara na kuwawekea miundombinu mizuri ya kuwawezesha kufanya biashara bila kubuguziwa.
Alisema Mwaka huu wananchi wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuweka malengo na mikakati itakayo wasaidia kujikwamua kiuchumi na kuacha kuilaumu serikali kwamba imebana hela na kushindwa kufanya kazi iliwapate fedha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...