Na Amina Kibwana-Globu ya Jamii.
Wizara ya ardhi,nyumba na maendeleo ya Makazi kupitia idara ya
nyumba imepewa jukumu la kusimamia mfuko wa mikopo ya Nyumba kwa
watumishi wa serikari kwa lengo la kuwawezesha watumishi wake
kujenga,kununua au kukarabati nyumba kupitia mkopo huo mwenye masharti
nafuu.
Akizungumza na waandishi wa habari
Mkurugenzi Idara ya nyumba Michael Mwalukasa amesema kuwa mfuko huu
ulianzishwa kwa ajili ya kusaidia na kuwawawwzesha watumishi wa serikali
wanaoishi mjini na vijijini kupata mkopo wa nyumba wenye masharti nafuu
kwa ajili ya kujenga au kununua nyumba.
Ameongeza
kuwa mfuko huo unatoa mikopo kuanzia milioni 20 kwa riba ya asilimia
tatu ambao muda wa juu wa kurejesha mkopo huo ni miaka thelasini(30)
katika kipindi cha utumishi kabla ya kustaafu au anapoacha utumishi kwa
sababu zozote zile.
Mwalusaka
amesema kuwa kuna sifa mbalimbali za kupata mkopo huu ikiwa ni pamoja
na mkopaji ni lazima awe mtumishi wa serikali, raia wa
Tanzania,aliyeajiriwa kwa masharti ya kudumu na kuthibitishwa kazini
pamoja na kuwa na hati ya kiwanja ambacho kitamuwezesha kupata mkopo kwa
ajili ya kujenga.
Kwa upande wake Mkurugenzi
msaidizi mikopo ya nyumba Lucy Kabyemera ameeleza faida za mikopo hiyo
kwa watumishi wa serikali ikiwa ni pamoja na kuwawezesha watumishi
kupata mikopp yenye riba nafuu, kuweza kumiliki nyumba kwenye maeneo
yenye hadhi,kuchochea kasi ya maendeleo kwenye miji na wilaya mbalimbali
pamoja na kutoa fursa kwa watumishi kumiliki nyumba kwa kadri ya
matakwa yao.
"Faida zipo nyingi sana kwani
pamoja na kunufaika na mikopo baadhi ya wakopaji pia wameendelea
kunufaika na ushauri wa kutumia technologia ya bei nafuu ya ujenzi
kutokana na tafiti zilizofanywa na taasisi iliyopo chini ya Wizara
(NHBRA)."
Kabyemera ameongeza kwa kusema kuwa
ujenzi wa nyumba unahitaji gharama nyingi hivyo ndio maana wameamua
kutoa mikopo hasa kwa watumishi wa serikali ili iweze kuwasaidia kwa
kuwapa fedha taslimu ya shilingi milioni 20.
Mfuko
wa Mikopo ya Nyumba ni moja wapo ya vyombo vilivyoanzishwa na serikali
mara baada ya nchi kupata uhuru mnamo mwaka 1963 kupitia waraka wa
watumishi wa serikali na.8 na badae kuendeshwa kupitia waraka wa
watumishi wa serikali na.4 wa mwaka 1965.
Mkurugenzi
wa Idara ya Nyumba Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw.
Michael Mwalukasa akizungumza na Waandishi wa Habari Leo Jijini Dar es
salaam kuhusu mfuko wa kuwawezesha watumishi wa Serikali kumiliki Nyumba
ambapo zaidi ya watumishi 2000 wameshanufaika na mikopo yenye riba
nafuu ya asilimia 3 ili kuwawezesha kumiliki nyumba bora. Kulia ni
Mkurugenzi Msaidizi Mikopo ya Nyumba Bi Lucy Kabyemera na Kushoto
Mkurugenzi
Msaidizi Mikopo ya Nyumba,Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Bi Lucy Kabyemera akifafanua kwa waandishi wa habari kuhusu faida
wanazopata watumishi wa Umma kutokana na mikopo inayotolewa na Serikali
ili kuwawezesha kumiliki makazi bora. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya
Nyumba Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Michael
Mwalukasa.Picha na Frank Mvungi-Maelezo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...