Shirika la Afya na elimu ya tiba Tanzania limefanikiwa kuendesha zoezi la uchangiaji damu kwa wagonjwa wenye selimundu (Sickle Cell) Siku ya Jumamosi Januari 21, 2017 katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala.
Kijana wa Umoja wa Mataifa (YUNA)  akichangia damu.
Zoezi hili limepewa ushirikiano mkubwa kutoka kwa vijana wakitanzania kutokana na idadi ya wachangiaji damu siku hiyo ambapo asilimia 95% ya wachangiaji damu ni vijana walio chini ya umri wa miaka 30 na asilimia 5% tu wakiwa juu ya miaka 30.

Mbali na uchangiaji damu vijana wengi walioshiriki wametumia vyema mitandao ya kijamii katika kuhamasisha watanzania kushiriki katika zoezi hili la uchangiaji damu.

Zoezi hili limelenga kuhusisha uchangiaji Damu kwa wagonjwa wa Selimundu na hivyo kuelimisha na kuchochea uelewa juu ya ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell) pia kuhimiza uboreshaji wa huduma za Afya Nchini kama inavyotajwa katika lengo la tatu katika malengo ya maendeleo endelevu duniani (Sustainable development Goals)

Zoezi zima liliandaliwa na kuendeshwa na Shirika la Afya na Elimu ya Tiba Tanzania (TAHMEF) kwa kushirikiana na Taasisi ya umoja wa wagonjwa wa Selimundu Tanzania, Vijana wa umoja wa mataifa (YUNA) na Lions Club ya Msasani Dar es salaam.

Shukrani Ziwafikie watanzania wote walioshiriki katika zoezi hili kwa njia mbalimbali ili kuokoa maisha ya watanzania wenzetu wenye uhitaji wa damu salama.

Zoezi hili linatarajiwa kuendelezwa tena kila baada ya miezi mitatu.
Muanzilishi wa shirika la Afya na Elimu ya Tiba (TAHMEF), Juliana Busasi (kushoto) akiwa na Muanzilishi wa Taasisi ya umoja wa wagonjwa wa selimindu Tanzania, Arafa Said (kati) na mmoja wa vijana waliochangia damu (kulia)
Lions Club Msasani wakikabidhi mahitaji ya zoezi la uchangiaji damu kwa wanachama wa TAHMEF.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...