Gari nne za kubebea wagonjwa na mbili za huduma zilizotolewa msaada na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Ulimwenguni (UNFPA) kwa ajili ya kutoa huduma katika Hospitali na vituo vya Afya Zanzibar zikiwa mbele ya Wizara hiyo Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
Kaimu Muwakilishi Mkaazi wa UNFPA Tanzania Dkt. Hashina Begum na Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo wakisaini makabidhiano ya magari manne ya kubebea wagonjwa na mawwili ya huduma yaliyotolewa na Shirika hilo katika sherehe zilizofanyika Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
Dkt. Hashina akimkabidhi Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo moja ya funguo za magari hayo kwenye sherehe zilizofanyika Wizarani kwake Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akiwa na Kaimu Muwakilishi Mkaazi wa UNFPA Dkt. Hashina Begum akilijaribu moja ya gari lilililotolewa msaada na UNFPA akwa ajili ya kuhudumia wagonjwa.
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo na Kaimu Muwakilishi wa UNFPA Tanzania Dkt. Hashina wakinyanyua moja ya vifaa tiba vilivyotolewa na UNFPA kwa ajili ya wodi ya mama wajawazito na watoto.

Picha na Makame Mshenga/Maelezo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...