Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi amewakabidhi hati miliki 810 za ardhi kwa wananchi wa Kijiji cha Kinywang’anga kilichipo Mkoani Iringa.
Wananchi hawa wamekabidhiwa hati hizo za umiliki wa ardhi baada ya kupimiwa maeneo yao ya viwanja na mashamba wanayoyamiliki na kuandaliwa hati miliki ambazo walikabidhiwa na Waziri wa Ardhi Mheshimiwa William Lukuvi kijijini hapo.
Katika tukio lingine Mheshimiwa William Lukuvi amezindua masijala ya ardhi ya kijiji cha Kinywang’anga Mkoa wa Iringa ili kuboresha huduma ya utoaji na uhifadhi wa hati miliki za ardhi.
Akizungumza na wakazi wa Kijiji hicho mara baada ya kuwakabidhi hati miliki zao za ardhi na kuzindua baraza hilo Waziri Lukuvi aliwasihi wananchi hao kuzihifadhi na kuzitunza hati zao hizo ili kuepukana na migogoro ya ardhi inayowakabili wananchi wengi wasio na hati miliki nchini.
Nae Mkurugenzi wa Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID) walioshirikiana na Serikali kuwezesha uandaaji wa hati miliki hizo Ndugu David Thompson amemshukuru Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi kwa kuja na kuwakabidhi Wananchi hati hizo na kuwaombaa Wananchi kuzitumia kwa maendeleo yao.
Wakazi wa Kijiji cha Kinywang’anga Mkoa wa Iringa wakiwa na hati zao za umiliki wa ardhi mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi (aliyevaa miwani) akifuatiwa na Mkurugenzi wa Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID) Ndugu David Thompson na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Richard Kasesela.
Baadhi ya hati miliki za ardhi zikiwa zinaandaliwa ili kugawiwa kwa wananchi wa Kijiji cha Kinywang’anga Mkoani Iringa.
Ndugu Yohanes Keng’ena na Mkewe Elizabeth Makang’olo wakipokea hati miliki ya ardhi kutoka kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi.
Bibi Catherine Abdallah akipokea hati miliki ya ardhi kutoka kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...