Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu ambaye pia ni Mkurugenzi wa huduma ya Upasuaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Bashir Nyangasa na Dk. Sun Long wakimfunga bandeji mgonjwa leo baada ya kumaliza kumfanyia upasuaji wa kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous Fistula) kwa ajili ya kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis).
Daktari bingwa wa upasuaji wa kifua, moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Wambura Wandwi (Kulia) na Dkt. Bingwa wa Upasuaji Hussein Hassan wakimfanyia mgonjwa leo upasuaji wa kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous Fistula) kwa ajili ya kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis). Kushoto ni Afisa Muuguzi wa chumba cha upasuaji Sr. Elina Mulenda.
Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu ambaye pia ni Mkurugenzi wa huduma ya Upasuaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Bashir Nyangasa (aliyevaa kofia ya pinki) akiwaonyesha kitu Dkt. bingwa wa upasuaji wa kifua, moyo na mishipa ya damu Wambura Wandwi (Kulia) na Dkt. Bingwa wa Upasuaji Hussein Hassan wakati wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous Fistula) kwa ajili ya kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis). Picha na Anna Nkinda - JKCI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...