Na Fredy Mgunda,Iringa

FAMILIA ya watu watano wenye ulemavu wa viungo wamemuomba mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rita Kabati kuendelea kuilea familia hiyo kama familia
yake.

Akizungumza na blog hii mmoja wa wanafamilia hiyo,Elias Mpogole ambaye ni mlemavu alisema kuwa mbunge huyo amekuwa akiwasaidia toka siku ya kwanza walipokutana naye katika kijiji hicho cha Lulanzi.

“Zamani tulikuwa tunaishi kwenye nyumba ambayo inavuja haina dilisha wala mlango pia tulikuwa tunalala chini lakini mbunge Kabati katusaidia nyumba nzuri kama mnavyoiona waandishi,katuletea magodoro,mashuka,blanket na sasa ameanza kutujenga choo cha kisasa na ameshawalipa mafundi pesa zote ndio maana tunaomba anendelee kuwa na sisi.”Alisema Mpogole

Mpogole alishukuru msaada waliopatiwa na kuwataka wadau wengine waweze kujitokeza zaidi kuwasaidia kuwapatia vyakula na radio za kuwezakusikiliza nyimbo za dini.

Kwa upenda wake mbunge wa viti maalum mkoa waIringa(CCM) Rita Kabati ametoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo ukarabati wanyumba kwa familia yenye watoto walemavu wanne wa kijiji cha Lulanzi kilichoko kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa. 

Mbunge wa viti maalum mkoa waIringa(CCM) Rita Kabati akiongea na familia ya watu watano wenye ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa wakati wa kuwasaidia msaada kukarabati nyumba yao pamoja na kuwapa vitu vingine vya kimsaada
Leah mwamoto mtoto wa mbunge wa jimbo la kilolo Vennance Mwamoto naye alishuhudia maisha magumu wanaoishi familia ya watu watano wenye
ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa na hapo aliposimama ndio choo kinachotumiwa na familia hiyo kwa sasa huku wakisubili ujenzi wa choo kipya kinachoendelea kujengwa kwa hisani ya mbunge Ritta kabati
Hivi ni baadhi ya vifaa vilivyoletwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rita Kabati kwa ajili ya kuwasidia familia ya watu watano wenye ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...