WATU takriban  39 wakiwemo wageni 15 wanahofiwa kuuawa katika shambulio lililotokea katika moja ya klabu ya burudani mjini Istanbul Uturuki usiku wa kuamkia mwaka mpya 2017.

Kwa mujibu wa waziri wa maswala ya ndani nchi hiyo, Süleyman Soylu alisema Mtu aliyekuwa amejihami kwa bunduki aliwafyatulia risasi watu waliokuwa wakijiburudisha katika mkahawa huo wa Reina majira ya saa saba usiku wakati ambapo watu walikuwa wakisherehekea kuingia kwa mwaka mpya.
Idanaiwa kuwa Mtu huyo aliingia katika klabu hiyo akijifanya kikaragosi kilichovaa mavazi ya Santa Claus na punde alianza kuwafyatulia risasi kiholela waliokuwepo ndani ya klabu hiyo ya burudani, hali iliyopelekea Baadhi yao kujirusha baharini kuepuka msusuru wa risasi zilizokuwa zinafyatulia na mtu huyo.Polisi mmoja ni miongoni mwa waliofariki.

Huku waliojeruhiwa wakikimbizwa hospitali, maafisa wa usalama wanaendelea kufanya upekuzi katika eneo hilo lakini muhusika wa shambilo hilo hajakamatwa bado.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...