Na Amina Kibwana,Globu ya Jamii.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt.Augustine Mahiga anatarajia kumpokea Waziri wa mambo ya nje wa Jamuhuri ya watu wa china Mh.Wang Yi anayetarajia kufanya ziara ya kikazi nchini Tanzania  Januari 9 Kwa lengo la kukuza  mahusiano mazuri baina ya china na Tanzania na kuangalia maeneo mapya ya ushirikiano wa kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam  msemaji wa Wizara ya mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mindi Kasiga amesema kuwa wakati wa ziara hiyo Waziri Wang Yi atakutana na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dkt. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na kufanya mazungumzo na Dkt Mahiga kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano wa Kimataifa baina ya Tanzania na China.

"Kwakuwa china iliichagua Tanzania kuwa miongoni mwa nchi nne barani Afrika zitakazo wezeshwa kupiga hatua kwenye maendeleo ya viwanda hivyo kupitia mpango huo tunatarajia viwanda takruban 200 vitajengwa au kuwekezwa nchini."

Amesema kuwa mbali na uendeshaji wa viwanda viongozi hawa watazungumzia miradi mingine ya miundombinu ambapo china imeahidi kuisaidia Tanzania ikiwa ni pamoja na maboresho makubwa ya Reli ya Tazara, Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo pamoja na ujenzi wa Reli ya Kati.

Aidha Mh. Yi anatarajiwa kuzungumza na mwenyeji wake kuhusu masuala ya ushirikiano wa Kimataifa ikiwa ni pamoja mageuzi ya Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa ambapo china inaunga mkono msimamo wa Afrika na  wa Tanzania kutaka Afrika ipewe viti viwili vya kudumu kwenye barala hilo na kepewa kura ya turufu, Masuala ya amani na usalama katika eneo la Afrika Mashariki pamoja na eneo la Bahari ya kusini mwa china.

Ameongeza kuwa mpango huo unaenda sambamba na mpango wa Taifa wa maendeleo wa mwaka  2016/2020 kupitia ahadi za Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh.John Pombe Joseph Magufuli wa kujenga Tanzania ya viwanda ifikapo mwaka 2020.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...