Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Msafara wa mwanamuziki wa bongo fleva, Ally Kiba  jana alisimamisha  jiji la Dar es Salaam kwa zaidi ya saa tatu mara baada ya kuwasili kutokea nchini Afrika kusini kuchukua tunzo yake ya Msanii bora barani Afrika.
Kiba ambaye aliwasili katika uwanja wa kimataifa wa JNA majira ya saa nane mchana na kulakiwa na wapenzi lukuki ambao aliambatana nao katika mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam. 
Msafara huo ambao ulianzia katika barabara ya pugu kasha kuingia katika barabara ya Mandela na kuwapa fursa wakazi wa buguruni na viunga vyake vya malapa na bungoni kushuhudia msanii huyo akiwa katika gari ya wazi huku akionyesha tunzo  yake huku wakazi hao wa jiji wakimshangilia.
Kiba alipita katika eneo alilozaliwa la Kariakoo mtaa wa Muheza na kumkabidhi mama yake tunzo hiyo na majirani zake ambao walipiga shangwe ya kutosha kutokana na mafanikio ya msanii huyo. 
Msafara wa msani huyo ulitoka kariakoo na kupita katika mitaa ya Msimbazi, Upanga na barabra ya Sarenda kasha kuelekea moja kwa moja katika hotel ya Double Tree Masaki kwa ajili ya mahojiano na waandishi wa habari.
 
 Ally Kiba akiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere  akitokea nchini Afrika Kusini mara baada ya kukabidhiwa tunzo yake ya MTV kama msanii bora wa kiume Afrika
 Kiba kielekea kwenye gari maalum aliyoandaliwa mara baada ya kuzngumza na mashabiki wake




 Ally Kiba akiwa na ndugu yake Abdul Kiba juu ya gari la wazi katika mita ya Buguruni
 Ally Kiba akimkabidhi Tunzo yake Mama yake mzazi maarufu kama Mama k
 Mama K ambaye ni mama mzazi wa Ally Kiba akionyesha Tunzo ya msani huyo juu. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...