Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Barclays Tanzania, Simon Mponji (katikati), akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi la kisasa la benki hiyo katika jengo la Shirika la Nyumba (NHC), mjini Morogoro mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed na kulia ni  Mjumbe wa Bodi ya benki hiyo, Dk. Suleman Mohamed.
 Mkuu wa Mauzo wa Benki ya Barclays Tanzania, (kushoto), akieleza kuhusu huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo katika tawi jipya Barclays la mjini Morogoro katika sherehe za uzinduzi wa tawi hilo juzi. Wengine kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji, Abdi Mohamed, mjumbe wa bodi, Dk. Suleman Mohamed na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Barclays, Simon Mponji . 
 Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Barclays Tanzania, Simon Mponji (wa pili kulia), akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi rasmi wa tawi jipya la benki hiyo mjini Morogoro. Wengine kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays, Abdi Mohamed na  Mjumbe wa Bodi ya benki hiyo, Dk. Suleman Mohamed.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...