Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uzalishaji wa Umeme kwa kutumia Maji ya Darakuta, Raphael Bapsl (katikati) akionesha moja ya chanzo cha maji kinachotumika katika kuzalisha umeme.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uzalishaji wa Umeme kwa kutumia Maji ya Darakuta, Raphael Bapsl (kushoto) akielezea mitambo ya kuzalisha umeme inavyofanya kazi katika kituo hicho kwa Mtaalam wa Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Emillian Nyanda (kulia).

Na Greyson Mwase, Manyara.

Imeelezwa kuwa kampuni ya uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji (Darakuta Hydro Power Project) iliyopo Babati mkoani Manyara inatarajia kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka Kilowati 370 hadi Megawati 1.3 zitakazoingizwa kwenye Gridi ya Taifa na kupunguza upungufu wa umeme nchini ifikapo mwaka 2021.

Hayo yalielezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Raphael Bapsl wilayani Babati mkoani Manyara wakati wa ziara ya wataalam wa nishati jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini katika wilaya hiyo, yenye lengo la kuangalia maendeleo ya miradi ya uzalishaji umeme na kubaini changamoto zake.

Akielezea historia ya mradi huo, Bapsl alisema kampuni yake ilianza kuzalisha umeme wa Kilowati 50 mwaka 1995 na kuongeza kuwa Aprili mwaka 2016 kampuni ilianza kuliuzia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) umeme unaoingizwa kwenye Gridi ya Taifa.

Alisema mbali na umeme huo kutumika kwa matumizi ya nyumbani ambao ni kidogo hususan katika shughuli za kilimo na ufugaji ili kujiongezea kipato, kampuni yake huuza umeme wa ziada kwa TANESCO ili kuongeza kiasi cha umeme katika wilaya ya Babati.

Alisisitiza kuwa ili Tanzania kuingia katika uchumi wa kati kupitia uwekezaji kwenye viwanda, nishati ya umeme wa uhakika inahitajika na kuendelea kusema kuwa kwa kutambua hilo kampuni yake imeweka mikakati ya muda mfupi na muda mrefu ili kuhakikisha inachangia katika ongezeko la umeme katika Gridi ya Taifa.
Mtaalam wa Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Emillian Nyanda (kushoto) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uzalishaji wa Umeme kwa kutumia Maji ya Darakuta, Raphael Bapsl mara baada ya wataalam wa nishati jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini kuwasili wilayani humo kwa ajili ya ukaguzi wa miradi ya umeme.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...