Na Mathias
Canal, Mwanza
Mkuu wa
Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha Mhe Alexzender Pastory Mnyeti amezuru kijiji cha
Misasi, Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza kutoa pole kwa familia ya Marehemu
Mzee Kayombo aliyefariki Dunia siku ya saa mbili usiku katika Hospitali ya
Rufaa Bugando, Mkoani Mwanza.
Mhe Mnyeti
ametoa salamu za pole kwa wakazi wa Kijiji cha Misasi kwa kumpoteza mshauri katika
kijiji hicho ambaye amekuwa nguzo kwa maendeleo ya kijiji sawia na utaratibu
wake wa kuhamasisha wananchi kupanda miti ili kukabiliana na mabadiliko ya
tabia nchi.
Mnyeti
ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya
Misungwi kabla ya uteuzi wake kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru ameeleza jinsi
alivyomfahamu Mzee Kayombo katika kuhakikisha jamii inasonga mbele katika
maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.
Mnyeti alisema kuwa Mkoa wa Mwanza umepoteza
mtu muhimu ambaye pia atakumbukwa kwa kazi njema alizozifanya wakati wa uhai
wake.
Dc Mnyeti, MD Kayombo na familia nzima ya Mzee Kayombo walipotembelea kaburi la Mzee Kayombo
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Alexzender Mnyeti (Kushoto), na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo wakiwa katika mazungumzo


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...