Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO), linawatangazia wakazi wa Maeneo ya Makongo na Goba jijini Dar es Salaam kuwa kuna tatizo la upatikanaji wa huduma ya Maji katika maeneo tajwa hapo juu, kuanzia siku ya Alhamisi tarehe 09/02/2017.

Sababu ya kukosekana kwa huduma ya Maji inatokana na hitilafu ya Pampu ya kusukuma Maji .Mafundi wetu wanaendelea na jitihada ili kuhakikisha huduma ya Maji inarejea.

Maeneo yaliyoathirika na hitilafu hii ni Goba Kunguru, Goda Kinzudi, Makongo Juu yote, Mbezi Juu eneo la Baraza la Mitihani na Eneo la Mnara wa Voda.

DAWASCO INAOMBA RADHI WANANCHI WA MAENEO HUSIKA KWA USUMBUFU UTAKAOJITOKEZA.

Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (BURE), Pamoja na Dawati la huduma kwa Mteja DAWASCO  Mkoa wa Kawe 0743-451861.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...