Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imezikutanisha Asasi za Kiraia zilizopo katika manispaa hiyo kwenye semina ya siku moja iliyolenga kuzijengea uwezo ili ziweze kutekeleza vyema shughuli zao katika kuwaletea maendeleo wananchi.
Mgeni rasmi katika semina hiyo ya siku moja iliyofanyika katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna uliopo katika manispaa ya Shinyanga alikuwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Akizungumza wakati wa kufungua semina hiyo Matiro amezitaka asasi za kiraia (NGO’s,CBO’) kuepuka kuwa sehemu ya kushiriki uovu katika jamii wakitumia mwamvuli wa asasi na kuzitaka kuepuka kuilaumu serikali badala ya kuishauri pale inapokosea.
“Serikali inatambua kazi nzuri zinazofanywa na asasi za kiraia katika kuisaidia jamii,nyinyi ni sehemu ya serikali,mnafanya kazi pamoja na serikali kuisaidia serikali,serikali yetu haiwezi kufanya kila kitu,hivyo haipendezi kuilaumu serikali,ishaurini pale mnapoona mambo hayaendi sawa”,amesema Matiro.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza ukumbini.Kulia ni Naibu meya wa manispaa ya Shinyanga Agnes Machiya
Mwenyekiti wa semina hiyo Mchungaji Dkt. Meshack Kulwa kutoka TCCIA Shinyanga akimkaribisha mgeni,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ili afungua semina hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na viongozi wa asasi za kiraia katika manispaa ya Shinyanga.Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...