Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh.Ali Hapi amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kuhakikisha anapeleka Mameneja pamoja na mashine za kielektronic(EFD),kwenye masoko kwa lengo la kudhibiti upotevu wa mapato unaoendelea. 

Ametoa agizo hilo jana  alipokuwa akisomewa taarifa ya mapato na matumizi ya Masoko na Mtendaji wa Kata ya Kijitonyama Bi. Elizabeth Minga  ambapo ilionesha upotevu mkubwa wa fedha kwenye masoko hasa soko la wamachinga lililoko Mwenge. 

Amesema fedha nyingi zinapotea kutokana na kutokuwepo utaratibu mzuri wa kukusanya mapato kwenye masoko. 

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya amepiga marufuku uanzishwaji wa vikundi vya kiholela vya kusimamia masoko ili kudhibiti upotevu wa mapato unaoendelea.

Kijitonyama ni Kata ya nne kati ya Kata kumi za awamu ya pili zinazotembelewa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo pamoja na utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi.
 Mkuu wa wilaya ya Kinondoni akiongea na Wamachinga wa soko la Mwenge ,Jijini Dares salaam
 Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ali Hapi akiendelea na ukaguzi soko la Mwenge, Jijini Dares salaam


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...