Jengo la Ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Igunga,Mkoani Tabora kulikofanyikia zoezi la upimaji wa afya kwa watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Igunga,Madiwani wa Halmashaurri hiyo pamoja na wananchi wa Halmashauri waliojiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF).
Na Jumbe Ismailly, Igunga
IDADI kubwa ya wananchi wa Wilaya ya Igunga, Mkoani Tabora wapo hatarini kupatwa na magonjwa ya shinikizo la damu kutokana na kutokuwa na utamaduni wa kupima afya zao hali ambayo inachangia miili yao kuwa na uzito mkubwa kupita kiasi.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Dk. Godfrey Mgongo aliyasema hayo wakati wa zoezi la kupima afya kwa watumishi,madiwani pamoja na wananchi ambao ni wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya (NHIF) wa Halmashauri ya wilaya hiyo lililofanyika kwenye viwanja vya Ofisi za Halmashauri hiyo. 
Baadhi ya wataalamu wa sekta ya afya waliokuwa wakitoa huduma za upimaji afya kwa watumishi wa Halmashauri ya Igunga,Madiwani pamoja na wananchi wa kawaida waliojiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF)ambapo iligundulika kuwa idadi kubwa ya wakazi wake wapo hatarini kupatwa na magonjwa ya shinikizo la damu kutokana na kutokuwa na utamaduni wa kupima afya zao na hivyo kuchangia miili yao kuwa na uzito mkubwa kupita kiasi.
“Kitu ambacho tumekigundua ni kwamba watumishi wengi au watu wengi wana uzito uliopitiliza,uzito mkubwa na hii inaweza ikapelekea ukapata magonjwa ambayo yatawaathiri katika maisha yao”alisema Dk.Mgongo.
Hata hivyo mganga mkuu huyo wa wilaya alivitaja vitu vilivyopimwa na wataalamu hao kutoka shirikisho la vyama vya magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza(TANCDA) kuwa ni uzito,shinikizo la damu,homa ya ini pamoja na kisukari na zoezi hilo limefanyika kwa siku nne ambapo lilianza kwa watumishi wa Halmashauri na baadaye huduma hiyo ilielekezwa kwa madiwani pamoja na wananchi.
Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Igunga,Mkoani Tabora wakiwa kwenye mkutano wa Baraza la kawaida la madiwani wa Halmashauri hiyo ambalo lilitumika pia kushiriki katika zoezi la upimaji afya kwa waliojiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF).(Picha Na Jumbe Ismailly)
Kwa mujibu wa Dk.Mgongo kati ya zaidi ya watumishi 60 wa Halmashauri hiyo waliopatiwa huduma ya upimaji wa afya, imegundulika kuwa tatizo kubwa linalowakabili watumishi hao ni uzito ingawa kuna tatizo la homa ya ini na ugonjwa wa kisukari ndiyo unaofuatia.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...