JE, UNATUMIA JIKO LA GESI KUPIKIA SOMA HII MUHIMU.

... na uchukue tahadhari ili isitokee kwako. Hili linaweza kuwa ni kosa la kawaida katika kila nyumba. 
JINSI ILIVYOTOKEA
Jiko la gas lilikuwa linamewaka na mapishi yakiendelea.
Mama akaona mende jirani na sink la kuoshea vyombo. Mara akachukua kopo la dawa ya mbu na kupuliza karibu na lile jiko la gas linalowaka.Ulitoka mlipuko mkubwa na ndani ya muda mfupi yule mama alikuwa ameungua kwa asilimia 65. 
Mumewe alikimbilia kuuzima ule moto na nguo zake nazo zilishika moto.Mumewe bado yuko hospitali akiuguza majeraha ya moto na bado hana habari kwamba mke wake alifariki alipofikishwa tu hospitali. 
Ni vema tukafahamu kuwa dawa zote za kuulia wadudu "Hit", "Marten", "heaven", "Raid" n.k. zina mchanganyiko wa madawa mengi yanayosababisha mlipuko mkubwa.Mchanganyiko huu wa madawa ni rahisi sana kusababisha mlipuko haraka sana. Tafadhali elimisha wanafamilia yako na rafiki zako kuhusu jambo hili, kwani yeyote yanaweza kumtokea.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...