Ni ile siku iliyosubiriwa ya kuumulika kibiashara mkoa
wa Simiyu ulioanzishwa mwaka 2012, ambao umejipambanua kuwa ‘mkoa darasa’, mintarafu suala zima la ujenzi wa viwanda
nchini.
Mwezi uliopita, Rais John Magufuli alipotembelea mkoa
huu, alipongeza juhudi zinazochukuliwa na mkoa huu chini ya mkuu wake, Anthony
Mtaka, katika kujenga uchumi wa viwanda na hivyo kuelekea kuifanya ndoto yake
ya Tanzania ya viwanda kutimia.
Kupitia Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN)
inayochapisha magazeti ya Daily News na HabariLeo pamoja na mitandao mbalimbali
ya kijamii, imeshirikiana na Mkoa wa Simiyu kuandaa Jukwaa la Biashara Simiyu likiwa na lengo la kuibua fursa za uchumi za mkoa huu darasa ambazo zitadadavuliwa na kuchambuliwa hii leo,
na hivyo kuwasaidia wawekezaji wa ndani na nje kujua ‘kunani’ Simiyu.
Mkuu wa Mkao wa Simiyu, Anthony Mtaka (kulia) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel katika Jukwaa hilo la Biashara Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara Mkoa wa Simiyu ambapo alilisitiza kuwa Simiyu itajengwa na wana Simiyu wenyewe na si kutegemea watu kutoka nje.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...