Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Watanzania wanaorudishwa nchini kutoka Msumbiji. Rwegasira amesema Uhusiano kati ya Tanzania na Msumbiji unaendelea kuimarika kila siku, hivyo aliwataka Watanzania wafuate Sheria za Uhamiaji za nchi hiyo kwani zoezi linalofanyika nchini humo halijawalenga Watanzania pekee bali raia wote wanaoishi na kufanya kazi bila kufuata taratibu za kisheria nchini humo. Aidha, amewataka wananchi kutolikuza tukio hilo bila sababu za msingi. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...